TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA NA UONE FAIDA YAKE

Kwa Habari au Tangazo lolote la Biashara tuwasiliane kwa Simu 0713 - 581741 au 0755 - 863097.Email: robadio8@gmail.com

Sunday, November 13, 2011

SUGU AVUNJA UKIMYA MBEYA ATAKA WALIOKAMATWA WAACHIWE HARAKA

Mkuu wa wilaya ya Mbeya Mheshimiwa Evans Balama mwenye shati la miraba ya samawati(Katikati) katika picha ya pamoja kabla ya Mheshimiwa Mbunge Joseph Mbilinyi Kuhutubia.

Mheshimiwa Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Bwana Joseph Mbilinyi akiwasihi wananchi kuwa watulivu na kwamba mgogoro umekwisha na utatuliwe kisayansi badala ya kisiasa na pia amewapongeza machinga kwa utulivu waliouonesha bila kupora bidhaa madukani.


Maelfu ya wananchi waliofika kuusikiliza mustakabali wa wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kama machinga kuendelea na biashara zao katika maeneo yao ya awali, wakati utaratibu ukiandaliwa na halmashauri ya jiji la Mbeya.

Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ), likiwasaidia Jeshi la Polisi kuweka hali ya amani na utulivu mara baada ya kuisha kwa mkutano uliofanyika katika kituo cha mabasi madogo ya abiria(daladala) eneo la Kabwe Mwanjelwa jijini Mbeya

Wananchi wakirudi makwao kwa furaha baada ya mgogoro uliodumu kwa siku mbili kumalizika, baada ya hotuba ya Mheshimiwa mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Bwana Joseph Mbilinyi.

No comments: