TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA NA UONE FAIDA YAKE

Kwa Habari au Tangazo lolote la Biashara tuwasiliane kwa Simu 0713 - 581741 au 0755 - 863097.Email: robadio8@gmail.com

Monday, January 28, 2013

HATIMAYE MAHAKAMA KUU YAMWACHIA LULU WA KANUMBA KWA DHAMANA

Elizabeth Michael maarufu kama Lulu
 Na Princess Asia
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo asubuhi imemuachia kwa dhamana msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayetuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba ‘The Great’ baada ya kupitia vifungu vya sheria.
Habari zimesema Lulu amepata dhamana kwa masharit kadhaa, ikiwemo kuacha hati yake ya kusafiria mahakamani, kuripoti mahakamani kila tarehe ya mwanzo ya mwezi na wafadhili wake waweke bondi ya Sh. Milioni 20.
Baada ya kusomewa dhaman, Lulu aliangua kilio mahakamani.
Hatua hiyo inakuja baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kubadilisha mashitaka ya mwanadada huyo kutoka kesi ya mauaji hadi kuua bila kukusudia.
Kutokana na mabadiliko hayo, hata kama atashindwa kesi, Lulu hatapewa hukumu ya kunyongwa kwa kuwa anatuhumiwa kwa kesi ya kuua bila kukusudia na kwa mujibu wa kifungu cha sheria, anaweza kufungwa maisha au miaka kadhaa.
Lulu anakabiliwa na tuhuma za kumuua The Great Kanumba aliyefariki dunia, Aprili 7, mwaka huu nyumbani kwake Vatican, Sinza Dar es Salaam.
Lulu aliyecheza filamu kadhaa na marehemu Kanumba waliyeibuka naye katika kundi la Kaole, Magomeni, anadaiwa alimsukuma Kanumba nyumbani kwake Sinza Vatican, ambaye pia inadaiwa alikuwa mpenzi wake.
Inaelezwa baada ya tukio hilo, Lulu alikimbia nyumbani kwa Kanumba na mdogo wa The Great, Sethi Bosco akaenda kuchukua gari kumpeleka kaka yake hospitali ya Muhimbili, ambako alipofika iligundulika amekwishafariki dunia.
Sethi alikaririwa akisema kwamba siku ya tukio, Lulu alikwenda kwao usiku wa manane na alipofika yeye (Sethi) alimuacha aongee na kaka yake. Sethi alidai aliwaacha sebuleni akaingia chumbani kwake na baadaye akasikia wameingia chumbani (kwa Kanumba).
Sethi alisema baada ya muda alisikia kelele za dalili ya ugomvi na baada ya muda Lulu alitoka kumwambia (Sethi) juu ya hali ya Kanumba kubadilika na kuwa mbaya.
Sethi alidai aliposikia hivyo akashituka na kwenda chumbani ambako alimkuta kaka yake katika hali mbaya, povu likimtoka mdomoni hivyo kuchukua hatua ya kumuita daktari wake, kabla ya kumkimbiza Muhimbili.
Lulu alikamatwa asubuhi ya kuamkia siku ya tukio hilo, linalodaiwa kutokea usiku wa manane na kuwekwa kizuizini katika kituo cha Polisi Oysterbay, Kinondoni, Dar es Salaam, kabla ya kufikishwa mahakamani.
Uchunguzi wa madaktari katika hospitali ya Rufaa ya Muhimbili ulisema pombe kali aina ya Jackie Daniels ilisababisha kifo cha mwigizaji huyo. 
Kifo cha Kanumba kiliwaumiza wengi, kwani msanii huyo alikuwa mahiri na kipenzi cha wapenzi wa filamu nchini.
Wapembuzi wa mambo wanasema huu ni msiba wa kwanza kuteka hisia za watu wengi zaidi, tangu kifo cha baba wa taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Oktoba mwaka 1999.

Imetolewa kwa Bin Zubeiry

Thursday, January 17, 2013

Presicion Air yazindua safari za Mbeya


Kaka Badi Darusi akipanda katika ndege no PW 401 ilionza safari zake kati ya Da - Mwanza na Mbeya

Kaka Allan Mihayo akiwa katika uwanja wa Ndege wa Songwa Mjini Mbeya tayari kwa safari ya kuelekea Dar

Kaka Darusi ndani ya Precion

Baadhi ya Abiria waliokua kwenye ndege no PW 401 wakiwa katika bara bara ya kukimbilia ndege katika Uwanja wa Julius Nyerere International Airport

Wakazi wa Mbeya  na Mikoa ya nyanda za juu Kusini jana walifuraia ujio wa ndege ya Precision iliyoanza safari zake kati ya Dar-Mwanza- Mbeya siku ya leo wakieleza kuwa ukombozi wa kiuchumi wa mikoa hiyo umewadia.

Hafla ya kupokea ndege hiyo ilihudhuliwa na umati mkubwa wa wakazi wa mkoani Mbeya waliofurika katika uwanja huo wa kimataifa wa Songwe huku Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Norman Sigala akiwaeleza wananchi kuwa wanatakiwa wautumia usafiri huo kujenga uchumi wa mkoa huo.

Ndege hiyo imewasili leo majira haya ya asubuhi maalumu kabisa kuzindua safari zake kufuatia kukamilika kwa uwanja huo wa kimataifa unaoweza kupokea ndege kubwa na ndogo.

Wadau wa usafiri wa anga mkoani humo wamefurahishwa na ujio wa ndege hiyo wakieleza kuwa utakuza na kuchochea uchumi wa Mkoa huo, pia walitoa wito kwa kampuni nyingine kujitokeza kuanzisha safari zao kwani wahitaji wa wasafiri ni wengi.

Wednesday, January 16, 2013

HALI CHADEMA SI SHWARI


582442 10152382144810063 1077508772 n 8b1ed

Na: Boniface Meena
KATIKA kuonyesha hali si shwari ndani ya Chadema, Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (Bavicha) wa chama hicho, Juliana Shonza amesema ameamua kumshtaki Mwenyekiti wake, John Heche kwa kumuita kuwa ni msaliti wa chama na kwamba anatumiwa na CCM na kuamua kumfukuza nafasi yake bila kutoa nafasi ya kusikilizwa.


Pia, amemlipua Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa akidai kuwa amefanya ufisadi ndani ya chama kwa kujikopesha Sh140 milioni ambazo hajazilipa hadi sasa.
Mbali na hilo, amemshukia Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwa kudai kuwa anatoa kauli za kukurupuka ambazo zinakiyumbisha chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Shonza alitoa kauli hizo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam juu ya tuhuma zilizotolewa na mwenyekiti wa Bavicha na kuhusu kufukuzwa kwake ndani ya chama akiwa na wenzake Mtela Mwampamba na Habibu Mchange.

“Heche na Mbowe wamenifedhehesha kwa kauli zao na wamenichafua na kunidhalilisha mbele ya umma wa Watanzania, hivyo nitapambana nao kuhakikisha haki yangu inapatikana,” alisema Shonza.

Shonza alisema kwamba yeye bado ni makamu mwenyekiti wa Bavicha na mwanachama halali wa Chadema kwa kuwa hadi anazungumza hakuwa amepewa barua ya kufukuzwa kwa kuwa kikao kilichotoa uamuzi huo ni batili.

Alisema kikao kilichoitwa ni cha kamati tendaji na kufikia maamuzi ya kumfukuza kilikuwa batili kwa kuwa katiba pamoja na mwongozo wa Bavicha ulikiukwa, kitu kinachosababisha aeleze kuwa uamuzi uliotolewa na kikao hicho yalikwishapangwa na viongozi wa kitaifa.

“Nasisitiza kwamba ni ukweli uliowazi kwamba ajenda na maazimio ya kikao hicho yalikwishaamuliwa hata kabla ya kikao hicho, kwa sababu taarifa za kufukuzwa kwetu zilikwishaanza kusikika kwenye mitandao ya kijamii kabla hata ya kamati tendaji batili,”alisema Shonza.

Alisema mkakati wa Heche na vibaraka wake umejikita kutukuza ukanda ndani ya chama waziwazi, akieleza kuwa watu waliofukuzwa ndani ya chama hicho wanatokea Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini haswa Mbeya wakati vijana wa Kaskazini wameachwa kwa madai kuwa wametoa ushirikiano.

“Natarajia kuomba ufafanuzi wa kikatiba juu ya shutuma zilizotolewa dhidi yangu na Heche kwa kuwaaminisha Watanzania uongo wake,”alisema Shonza.

Kuhusu Mbowe
Alisema kuwa amesikitishwa na kauli ya kiongozi wake huyo katika baadhi ya vyombo vya habari kwamba, madai aliyoyatoa ni ya kitoto kwani ni kitu cha kushangaza kwa kuwa yeye Juliana hayajui ni madai gani hayo.

Alisema kama madai ambayo Mbowe anadai ni ya kitoto ni ya yeye kuhoji kwa nini chama hakiweki akiba kwenye akaunti kwa ajili ya uchaguzi wa 2015 kama ilivyokubaliwa kwenye baraza kuu basi itakuwa ni ajabu.

Kuhusu Dk Slaa
Alisema inashangaza kwa mwenyekiti wa chama anafumbia macho hatua ya Dk Slaa kujikopesha pesa ya ruzuku ya Watanzania zaidi ya Sh140 milioni, kwani ni kinyume na utaratibu uliopo.

Habari hii kwa hisani ya Mjengwa Blog

Wednesday, September 12, 2012

WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU WALAANI MAUAJI YA MWANGOSI NA KUFUNGIWA KWA GAZETI LA MWANAHALISI


Baadhi ya Washiriki wa kongamano la kupinga mauaji ya Daudi Mwangosi na kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi wakifatilia Mjadala katika Kongamano hilo




 Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Bi. Ussu Mallya akiwaongoza washiriki wa Kongamano la Kulaani mauaji ya Daudi Mwangosi na Kufungiwa kwa gazeti la Mwana Halisi kumuombea Marehemu Daudi mwangosi. Kongamano hili limefanyika katika viwanja vya Mabadiliko vilivyopo katika ofisi ya Mtandao wa Jinsia Tanzania.


 Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar - es - Salaam Dr. Ayoub Rioba  akielezea umuhimu wa kulindwa kwa waandishi wa habari wakati wakitekeleza wajibu wao.


 Mmoja wa wanajopo wa Kongamano la kupinga Mauaji ya Daudi Mwangosi na kufungiwa kwa gazeti la MwanaHalisi

Mwanasheria kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Ndg Harold Sungusia akielezea masuala ya haki za binaadamu na hali halisi ya mauaji yanayotokea hivi sasa nchini



Baadhi ya washiriki wa semina za Jinsia na Maendeleo GDSS wakionyesha mabango yaliokua na jumbe mbali mbali wakati wa kongamano la kupinga mauaji ya Mwandishi Daudi Mwangosi na kufungiwa gazeti la Mwana Halisi


Katibu Mkuu wa jukwaa la Wahariri Ndg, Nevile Meena akionyesha msisitizo wakati akielezea hali halisi ya waandishi wa habari Nchini

Wednesday, August 22, 2012

Mwakilishi wa Tanzania kwenye fainali Miss East Africa Belgium


Miss East Africa Belgium 2012
Mwakilishi wa Tanzania kwenye fainali Miss East Africa Belgium yatakayofanyika tarehe 1 September 2012, Miss Juliana Pierre 


Muunge mkono mwakilishi wetu huyu kwenye Fainali husika kwa kuongeza  idadi ya kufahamika kwake.
Juliana anaomba uingie kwenye ukurasa wake wa (Face book) na kubonyeza kitufe cha “like” kwa anuani hii: https://www.facebook.com/JulianaPierreFinalisteMissEastAfricaBelgium2012
Tangaza Vipaji Vyetu,Tangaza Utalii Wetu, Tangaza Tanzania.
------------------------------------------------

Thursday, August 9, 2012

MALAWI YATOA MSIMAMO KUHUSU MPAKA WA ZIWA NYASA

At around the time of independence quite a few people in Tanzania wanted to claim a huge part of Lake Malawi or Lake Nyasa . Cool heads eventually prevailed, as most Tanzanians, including the legendary President Julius Nyerere, understood the importance of respecting boundaries emanating from colonial times.


During most of Dr Kamuzu Banda’s rule, Tanzania never really pushed this crazy idea of dividing up the lake. The issue was almost forgotten during the rule of Dr Bakili Muluzi and thereafter. In fact, Dr Bingu wa Mutharika commissioned a company to start exploring oil in the lake. Tanzania said nothing at that time.



Now we have a new president and all of sudden the Tanzanians are demanding that our government stop all exploration activities in the lake until all border issues have been clarified. Why now?



Folks, there is a reason why we have tradition. Tradition may appear useless and outdated but it is important because it usually become established after a long experience. In politics there is what is known as ‘presidential protocol’. These are small things which over the years have proven to be niceties a president must or must not do in order to represent his/her country correctly.



Test for President Joyce Banda to diplomatically manage the dispute on the boundary

You would think some of them are not important but they are. Here are a few of them – presidents never bow for other presidents in public; presidents never escort anybody to their car; presidents walk with their arms spread outwards apparently projecting power and being in control; presidents usually put on a solid color (one color) necktie because it portrays power; when two presidents greet each other while facing the camera, each of them jostle to be on the right side so that his palm will face the camera- another sign of power, apparently; when in company of other presidents, they try to be the last one to enter the door – a fatherly gesture; there is an interesting video clip of Chairman Yassier Arafat and PM Ehud Barak jostling to be the last one to enter a room at Camp David. The sight of President George W Bush gently pushing PM Gordon Brown into Number 10 Downing Street before himself angered some British political experts.



Statesmanship is a game because image is everything in international politics. A country’s image depends a lot on the demeanor of its leader. President Barak Obama likes to pat other leaders on their back after greeting them; you thought that was an unplanned coincidence? Just remember, how your father used to pat you on the back when you were a good boy!



It is said that Bill Clinton failed to get a good deal at his summit with Boris Yelsin in Moscow because President Clinton having sprained his ankle arrived in Moscow on a wheelchair. The sight of a sick American president is said to have psychologically emboldened Boris Yelsin. Ghana is said to have regained its respect in West Africa when President J.J. Rawlings arrived at the 25th Organization of African Unity meeting in Togo in July 2000 in a military uniform portraying a very youthful image.



The presidency is acted on a world stage. What a president says and does is very important!
When Joyce Banda took over the presidency, she made it appear like Malawi will now be doing everything the donor community tells her to do. In fact some British newspapers were so pleasantly surprised with this that they called us ‘a donor fearing nation’.



President Joyce Banda went to London and even bowed before Queen Elizabeth, a very strange gesture considering that both are heads-of-state. Well, all these words and actions have now collectively given an image of a weak leadership in Malawi. The world has sensed blood. Now Tanzania has decided it is time to split up the lake. Notice that they did not bring up this crazy idea when Muluzi or Mutharika were in charge.





                                                     Nyasa (Malawi)

If we dignify Tanzania’s unreasonable request, one wonders what the next thing will be. Are they now going to claim Chitipa? Will Mozambique now claim Mulanje Mountain?



Government must make clear that no part of Malawi is up for discussion – full stop! It is time to show strength. Tell Tanzania that Lake Malawi was, is and will always be Malawian.



Surprisingly, after all these arrogant statements by the Tanzania government, our government’s response is at best a whimper. The minister of foreign affairs has issued a statement saying the issue will be settled ‘amicably’. Really, Mr. Minister? What could be an amicable statement? Are you planning to even dignify Tanzania’s unreasonable demand? Do you plan to divide up the lake? How can you have an amicable settlement to an unreasonable demand?








Monday, July 30, 2012

GAZETI LA MWANAHALISI LAFUNGIWA KWA MUDA USIOJULIKANA

 
 
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imelifungia kutochapishwa gazeti la MwanaHalisi kuanzia 30 Julai, 2012 kwa muda usiojulikana kutokana na mwenendo wake wa kuandika habari na makala za uchochezi, uhasama na uzushi likiwa na nia ya kusababisha wananchi kukosa imani na vyombo vya dola hali inayoweza kuhatarisha amani na mshikamano uliopo nchini.
              Katika matoleo yake hivi karibuni, gazeti la MwanaHalisi toleo Na. 302 la Jumatano Julai, 11 – 18, 2012 na toleo Na. 303 la Jumatano Julai 18 – 24, 2012 na toleo Na. 304 la Jumatano Julai 25 hadi 01 Agosti, 2012 na mengine yaliyotangulia yamekuwa yakichapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii.
              Mhariri wa gazeti la MwanaHalisi, ameitwa na kuonywa mara nyingi, lakini hataki kukiri kuwa maudhui ya makala zake hazina tija kwa jamii, pia hazifuati weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.
              Mhariri, mara zote katika utetezi wake amekuwa akinukuu kifungu cha 18 cha Katiba ya nchi yetu ambacho kinatoa uhuru wa kutoa maoni na kwa makusudi kutonukuu kifungu cha 30 cha Katiba hiyo kinachoweka ukomo wa uhuru.
              Uamuzi wa Serikali
              Serikali imeamua kulifungia kutochapishwa kwa muda usiojulikana gazeti la MwanaHalisi, kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976, kifungu Na. (25) (i), adhabu hiyo itaanza tarehe 30 Julai, 2012 kwa mujibu wa Tangazo la Serikali (Government Notice) Na. 258 lililochapishwa katika Gazeti la Serikali na kutolewa jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Julai, 2012.
              Serikali inawataka wamiliki, wahariri na wanahabari kuzingatia sheria, uzalendo, weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari katika kutekeleza wajibu wa kuhabarisha, kuelimisha na kutoa burudani kwa wananchi.
              Kama ilivyoelezwa Bungeni wakati wa kuwasilisha Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo hivi karibuni waandishi na watangazaji wa habari wanatakiwa kuhakikisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoandaa vinazingatia  taaluma na kuweka mbele maslahi ya Taifa letu na uzalendo. Uhuru na haki ya vyombo vya habari uendane na wajibu.
              Kuanzia sasa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya vyombo vya habari ambavyo kwa maksudi vitatoa taarifa za uchochezi ambazo zitahatarisha hali ya amani na utulivu uliopo nchini mwetu.
Imetolewa na
OFISI YA MSAJILI WA MAGAZETI
WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

30 Julai, 2012