TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA NA UONE FAIDA YAKE

Kwa Habari au Tangazo lolote la Biashara tuwasiliane kwa Simu 0713 - 581741 au 0755 - 863097.Email: robadio8@gmail.com

Saturday, April 14, 2012

OMARY MAUNDA AZIKWA KWA HESHIMA ZOTE ZA KIJESHI






Umati wa Watu waliojitokeza katika Mazishi ya Marehemu Omary Maunda aliefariki kwa Ugonjwa wa kupungukiwa damu mara kwa mara Mwilini.Omary Maunda ambae alikua mwanafunzi wa zamani wa Ununio Boys Islamic High School (2001 -hadi 2003.Mpaka anakufa Marehemu Omary Maunda alikua mtumishi wa Jeshi la Magereza mwenye cheo cha Afisa mkaguzi Msaidizi(Assistant Inspector.Ameacha mke na mtoto mmoja



Mwili wa Marehemu Omary Maunda ukitolewa katika jeneza kwa ajili ya Mazishi yake.Omary Maunda ambae alikua mtumishi wa Magereza mwenye cheo cha Afisa Mkaguzi msaidizi.

Kaburi alilohifadhiwa Marehemu Omary Maunda kama linavyoonekana




Baadhi ya Wanafunzi wa zamani wa Ununio Boys High school bwana Seif Mikoi alievaa tshirt nyekundu na Abdulatif Said mwenye shati jeupe wakishiriki kikamilifu katika mazishi ya mwanafunzi mwenzao wa zamani Marehemu Omary Maunda.Omary Maunda amefariki kwa ugonjwa wa kupungukiwa damu mara kwa mara mwilini



Askari wenye vyeo vya Afisa mkaguzi msaidizi wa Magereza wakiwa wamebeba Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Omary Maunda ambae mpaka anakufa alikua na Cheo cha Afisa Mkaguzi Msaidizi wa Mgereza. Omary Maunda ameacha Mke na mtoto mmoja.





Askari Magereza wakipokea Mwili wa Askari mwenzao Marehemu Omary Maunda kutoka kwa Waumini wa dini ya Kiislam waliokuwa wameubeba kwa ajili ya kupisha taratibu za mazishi za kijeshi kuendelea





Askari wa Jeshi la Magereza wakipiga Risasi Hewani kama Ishara ya Heshima kwa askari mwenzao aliefariki dunia Marehemu Omary Maunda ambae alikua ni mwanafunzi wa zamani wa Ununio Boys High School.





Askari wa Jeshi la Magereza Wakiwa katika gwaride maalumu la heshima kwa ajili ya Askari mwenzao aliefariki dunia marehemu Omary Maunda.Marehemu Omary Maunda alifariki kwa ugonjwa wa Kupungukiwa damu mara kwa mara.

No comments: